Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Shaka Hamdu Shaka
Shaka amesema kwamba siasa safi inahusisha uzalendo, utu, heshima na kuweka mbele maslahi ya Taifa kuliko chochote ambapo Rais Samia, amekuwa ni kielelezo katika hili na ameendelea kuthibitisha dhamira yake ya kuijenga Tanzania moja yenye ustawi kwa wananchi wote.
Aidha, amebainisha kuwa Ibara ya 118 ya Ilani ya uchaguzi ya CCM inaeleza katika kipindi cha miaka mitano ijayo, Chama Cha Mapinduzi kitaendelea kuheshimu na kulinda misingi ya demokrasia na haki za binadamu kwa ajili ya kudumisha umoja, amani na ustawi wa Taifa kwa kuzingatia katiba ya nchi.



