Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Siku 7 bila ya Mo, CCM, CHADEMA, ACT, CUF wamlilia

Alhamisi , 18th Oct , 2018

Ikiwa imetimia siku ya saba tangu kupotea kwa mfanyabiashara na bilionea kijana maarufu Afrika Mohamed Dewji wanasiasa mbalimbali bila kujali itikadi za vyama vya siasa wameoneshwa kuguswa kwa hisia tofauti juu ya tukio hilo.

Mfanyabiashara Mohamed Dewji

Www.eatv.tv imefuatilia baadhi ya wanasiasa wenye nguvu kubwa ya ushawishi kwenye mitandao ya  kijamii nchini wanaotokea Chama cha Mapinduzi CCM, Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Act- Wazalendo pamoja na Chama Cha Wananchi (CUF).

Kwa upande wa CCM, miongoni mwa watu ambao walionesha kuguswa na tukio la kupotea kwa Mohamed Dewji ni Waziri wa zamani wa Mambo ya ndani ya nchi, Dkt Mwigulu Nchemba, ambaye siku ya tukio la kutekwa kwa Mo Dewji aliandika “Comrade,this too shall pass..Nakuombea uwe salama”, akimaanisha kuwa hili nalo litapita na kumuombea kwa Mungu mfabiashara huyo apatikane.

Kada mwingine wa CCM aliyeonesha kuguswa na tukio hilo ni Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye ambaye nae alichapisha picha ya Mo Dewji na kuandika ujumbe “ooh GOD na kuweka alama (emoji) ikionesha akibubujikwa na machozi.

Mbunge wa Nzega mjini, Hussein Bashe ambaye nae aliandika “inasikitisha na kustua tukio hili la @moodewji kutekwa aina hii ya uhalifu inaota mizizi, ana familia ana watoto ana ndugu,  tuendelee kumuombea kwa Allah na kila mmoja wetu kutoa taarifa yoyote atakayopata ambayo itasaidia kumpata akiwa salama Allah amlinde."

Mbali na wabunge hao CCM, Mbunge mwingine wa CHADEMA ambaye ni Waziri kivuli wa mambo ya  ndani ya nchi, Godbless Lema ambaye nae wakati tukio hilo likitokea, aliandika “kama Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani,ninafuatilia kwa karibu suala la kutekwa mfanya biashara Mo Dewji.”

Mbunge mwingine ni, Zitto Kabwe wa kigoma Mjini kupitia Chama cha ACT- Wazalendo ambaye nae amekuwa akiandika mara kwa mara juu ya tukio hilo na maelezo yake akiyaelekeza kwa vyombo vya ulinzi na usalama nchini.

Na Kwa upande wa Chama Cha wananchi CUF upande wa Zanzibar, tukio hilo limemuibua Mkurugenzi wa Mambo ya Nje na Mahusiano ya kimataifa ya chama hicho, Ismaili Jussa ameandika "leo ni Siku ya 7. hatuwezi kukaa Kimya.”

Mpaka sasa hakuna mtu yeyote aliyethibitika kuhusika na tukio la kutekwa kwa mfanyabiashara huyo maarufu nchini licha ya jeshi la polisi kuwahoji watu 26.

HABARI ZAIDI

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea