Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Sugu atinga Bungeni na kuzua majibizano

Jumatatu , 21st Mei , 2018

Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi maarufu kwa jina la Sugu, leo amehudhuria kikao cha Bunge I ikiwa ni mara ya kwanza tangu aachwe huru kutoka jela kwa msamaha wa Rais.

Akiwa Bungeni humo Sugu alipata fursa ya kuuliza swali ambalo lilizua majibizano kati yake na Mwenyekiti wa Bunge Andrew Chenge ambaye ndiye aliyekuwa akiendesha Bunge kwa leo.

Baada ya Sugu kusimama na kuwasha kipaza sauti chake alianza kwa kusema …. “Ahsante Mheshimiwa mwenyekiti, niwatakie mfungo mwema ndugu zangu Waislamu ndani ya Bunge na nchi nzima, kwa wale ambao ni viongozi watumie mwezi huu kujitathimini......(Mwenyekiti akamkatisha na kumwambia “Unaonaje ukiuliza swali”.

Sugu akaendelea kwa kusema.... “Sheria hii pamoja na sheria nyingine mbovu za habari, sio tu inabana kupata habari, pia inatumika kufunga watu jela hovyo kisiasa, mfano mimi nilifungwa kwa kujadili na wananchi wangu taarifa za watu kupigwa risasi, watu kutekwa, watu kuokotwa kwenye viroba, watu kutokuwa na uhuru wa kuongea na kadhalika, kitu ambacho sio mimi tu niliyokijadili, ni kitu ambacho kilishajadiliwa ndani ya Bunge hili, na pia maaskofu wakatoliki ….....Mwenyekiti akamkatatisha na kumwambia “uliza swali...”

Sugu akaendelea.. Swali, ni lini sheria hii itafutwa ili kulinda katiba ya nchi hususan ibara ya 18, mfano.....Mwenyekiti akamkataisha na kumzimia mic akimwambia “ahsante umeeleweka”.

Baada ya hapo Naibu Waziri Mhandisi Edwin Ambandusi Ngonyani alisimama na kuanza kujibu swali la Sugu akisema kwamba sheria zote serikali ina mechanisim ya kuzitazama wakati wowote, na kumtaka kuonana na Mbunge huyo ili waweze kupeana miongozi wapi pana ugumu juu ya sheria hizo.

 

 

HABARI ZAIDI

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu