Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

TANESCO yakabidhi mil 30 kwa wabunifu umeme

Jumanne , 18th Jun , 2019

Shirika la umeme Nchini TANESCO limetekeleza agizo la Rais John Magufuli alilolitoa Juni 13 Ikulu mara baada ya kukutana na wabunifu wa umeme kutoka mkoani Njombe la kuwataka kuwatembelea, kuwatambua, kuwapa ushauri wa kitalaamu.

Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco akimkabidhi pesa mmoja wa wabunifu

Wabunifu hao wamekabidhiwa fedha taslimu Sh. 5 milioni pamoja na hundi ya Sh. mil 10 kila mmoja huku lengo kuu likiwa ni kuthamini na kutambua ubunifu na jitihada ambazo zimechukuliwa na watu hao katika kutimiza ndoto zao.

Akizungumza mbele ya umati wa wakazi wa kijiji cha Lugenge wakati akikabidhi hundi ya fedha yenye thamani ya mil 10 pamoja na fedha taslimu mil 5 kwa wabunifu wote wawili akiwemo John Fute maarufu Dr. Pwagu na Laniel Ngailo Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO, Dr. Titho Mwinuka amesema serikali itaendelea kuthamini na kutoa usaidizi wa kila hali ili kufikisha ndoto panapo stahili.

Kwa upande wao wabunifu hao wamesema imekuwa kama ndoto kwa Rais kutambua uvumbuzi na ubunifu wanaoufanya na kuamua kuwaunga mkono kwa kuwapa watalaamu na fedha ili kuboresha huduma zao huku pia wakionyesha hisia zao juu ya hatua ya TANESCO kuwakabidhi fedha taslimu mil 5 na hundi ya mil 10 kila mmoja kama ambavyo iliahidiwa.

Mara baada ya agizo naibu katibu mkuu, Mratibu wa masuala ya habari na maarifa kutoka COSTECH ndugu Deusdedith Lenard anasema agizo hilo litatekelezwa haraka iwezekanavyo kwa kuanza mara moja uboreshaji wa kiota hicho cha ubunifu kilichopo nyumbani kwa Pwagu ili kiweze kutumiwa na watu wengi kubuni vitu mbalimbali huku baadhi ya Wananchi wakizungumzia umuhimu wa Huduma ya Nishati ya Umeme.

Timu hiyo imewasili ikiwa na watalaamu kutoka TANESCO, COSTECH, REA, Wizara ya maji, Ewura na Mamlaka za Bonde la mto Rufiji na Nyasa huku kila mmoja akitazama namna ya kuwasaidia wabunifu hao ambao wamekumbana na changamoto nyingi mpaka kufikia hapo.
 

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa