Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Tanzania tunasalitiana wenyewe" – Anna Mghwira

Jumanne , 11th Dec , 2018

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mama Anna Mghwira amesema kitendo cha bidhaa za Tanzania kushindwa kufanya vizuri kwenye masoko ya kimataifa ni kutokana na usaliti uliopo, na hivyo kusababisha mambo mengi kutoenda mbele.

Akizungumza na www.eatv.tv, Mama Mghwira amesema watu wanaotumwa kwenda kufanya kazi za kuitangaza Tanzania na kujifunza mapya ili walete tija nchini huwa wasaliti na kuishia kuangalia mambo yao binafsi, huku akitolea mfano wa zao la kahawa linalozalishwa mkoani humo kuwa ndiyo namba moja kwa ubora lakini haipo kwenye soko la dunia.

“Tanzania tunajisaliti wenyewe, wasaliti halisi wapo na walitangulia huko nyuma, walishindwa kulitetea taifa, mtu anaenda kwenye mikutano ya kimataifa ametumwa na nchi anaishia kwenda madukani kutembea kuona vitu, mambo ya kipuuzi kabisa, pole pole Tanzania inapotea, hatujui aliyemtuma anamfuatailia kiasi gani, na kila siku watu wanaenda nje wakirudi nyumbani hawafanyi”, amesema Mama Mghwira.

Mama Mghwira ameendelea kusema kwamba watu hao wakiwemo wawakilishi wetu ambao wana fursa kubwa ya kwenda nchi zingine mara kwa mara na kujifunza, huwa hawazingatii walichokiendea, na wakirudi wanashindwa kuwasilisha walichojifunza.

“Wawakilishi wetu ambao ni wabunge na wana dhamana kubwa, wana fursa kubwa sana ya kwenda nje kuona ili kuja nyumbani na kuboresha, lakini wanaishia kuja na kiatu kipya, tena akija anaringa nacho kweli, unaishia kuwahurumia tu”, amesema mama Mghwira.

Kutokana na hilo Mama Mghwira amesema anaandaa mfumo ambao utatangaza mkoa wa Kilimajaro na Tanzania kimataifa, ambao kila mkazi wa mkoa huo na wengineo watapata fursa ya kuutangaza kwa namna yake.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali