Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Tanzania yakabiliwa na mabadiliko ya tabia nchi

Ijumaa , 5th Aug , 2022

Tanzania inaendelea kubainishwa kama nchi iliyo hatarini kukabiliwa na athari za mabadiliko tabia ya nchi inayotishia ukuaji wa uchumi na maendeleo endelevu huku suluhisho ikitajwa kuwa ni kutumia nishati mbadala ikiwa ni mfumo salama wa matumizi ya Nishati.

Ripoti ya Mipango endelevu ya Wentworth ya mwaka 2021 inaitaja Gesi asilia kama mbadala wa vyanzo vya nishati zinazochafua mazingira ikiwemo mafuta mazito na diseli ambayo itakuwa fursa ya kuiwezesha Tanzania kukua kiuchumi.

Taarifa hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Wentworth Katherine Roe wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa Ripoti ya Mipango endelevu ya Wentworth iliyofanyika jijini Dar es salaam inayoelezea mtazamo wa makakati endelevu unaowiana na malengo ya maendeleo endelevu SDGs ya kimataifa inayozingatia nguzo tano ikiwemo kuwezesha mabadiliko ya nishati na utawala dhabti wa mazingira,kijamii na utawala.

Kwa sasa mahitaji ya gesi nchini yanatumika kwa kiasi kikubwa kuzalisha umeme kwa asilimia 79 ikifuatiwa na mahitaji ya viwanda kwa asilimia 21 na kisha matumizi ya nyumbani na gesi asilia iliyosindikwa.

Kwa Mujibu wa taarifa yake amesema Gesi inayozalishwa na Mtambo wa kuzalisha gesi wa Mnazi bay iliopo katika Bonde la Ruvuma Kusini mwa Tanzania imechangia asilimia 50 ya mahitaji ya gesi asilia nchini ambapo hatua hiyo imesababisha lita bilioni 4.6 za dizeli na mafuta mazito kuacha kutumika kutokana na matumizi ya gesi asilia

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi