Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Tanzania yaziunganisha benki mbili kuwa moja

Jumatano , 16th Mei , 2018

Benki Kuu ya Tanzania BoT, imeridhia uamuzi wa kuiunganisha Benki ya Twiga Bancorp Ltd na ile ya Tanzania Postal Bank Public limited Company (TPB Plc), ili iwe benki moja yenye nguvu ambayo utendaji wake utakuwa chini ya usimamizi na uendeshaji wa TPB Plc, uamuzi ambao utaanza Mei 17, 2018

Hayo yamebainishwa na Naibu Gavana wa Benki Kuu Dkt. Bernard Kibese wakati alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam leo Mei 16, 2018 na kusema benki hiyo ya Twiga Bancorp iliyokuwa chini ya usimamizi wa benki kuu kwa takribani ya miaka miwili, ambapo mali za wateja na madeni ya benki hiyo kwa sasa yatasimamiwa na benki ya Tanzania Postal Bank Public Limited Company.

Dkt. Kabesema amesema uamuzi huu umechukuliwa ili kuboresha uangalizi na utendaji wa benki zinazomilikiwa na serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania. Benki Kuu ya Tanzania inapenda kuuhakikishia umma kuwa itaendelea kulinda maslahi ya wenye amana katika mabenki kwa lengo la kuleta ustahimilivu katika sekta ya fedha.

Pamoja na hayo, Naibu Gavana Kibese amesema hatua kama hiyo itachukuliwa pia kwa benki nyingine za serikali ambazo ufanisi wake hautokuwa wa kuridhisha, kwani nia ya serikali ni kuwa na benki moja kama sio chache zinazofanya vizuri, malengo ambayo Rais Dkt John Pombe Magufuli amekuwa akisisitiza mara kwa mara.

Kwa upande wake Meneja Uendeshaji wa Bodi ya Bima ya Amana, Bi Rosemery Tenga amewataka walikuwa wateja katika benki ambazo zipo chini ya BOT kufuata mitaji ya benki hiyo kuyumba kwenda katika benki hizo na utaratibu wa malipo utafanyika chini ya usimamizi wa bodi ya Amana.

Uamuzi huo wa BoT umetokana na benki ya Twiga kuwa na upungufu mkubwa wa mtaji ambapo ni kinyume na matwaka ya sheria ya mabenki na taasisi za fedha ya mwaka 2006 na kanuni zake ambapo kwa wakati huo ilihatarisha usalama wa sekta ya fedha.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi