Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Theresa May akubali kung'atuka

Ijumaa , 24th Mei , 2019

Waziri Mkuu wa Uingereza, Bi Theresa May ametangaza kuwa atajiuzulu wadhifa wake ifikapo Juni 7, 2019.

Bi May amehudumu katika  nafasi hiyo kwa muda wa miaka mitatu, ambapo amesema muda uliosalia kabla ya kuachia ngazi utumike kwa ajili ya mchakato wa kumpata Waziri Mkuu mpya wa serikali ya nchi hiyo.

Waziri Mkuu huyo anayetokea katika chama cha Conservative amekumbana na ukosoaji mkubwa kutoka kwa miongoni mwa wabunge wake kutokana na mpango wake wa kujitoa katika muungano wa mataifa ya Ulaya, maarufu kama 'Brexit' ambapo ushawishi wake umeonekana kuhusisha vyama vingine.

Katika taarifa yake leo Ijumaa, Bi May amesema kuwa ili kufanikisha mpango wa Brexit, ni lazima mrithi wake aimarishe ushawishi na maelewano mazuri katika bunge.

"Makubaliano hayo yanaweza kufanikiwa tu endapo kila upande ulio katika mdahalo ukiwa tayari kuelewana", amesema Bi May katika hotuba yake.

"Mimi nafanya hivyo bila dhamira yoyote, lakini kwa shukrani kubwa na ya kudumu kuwa na fursa ya kutumikia nchi ninayoipenda", ameongeza.

Naye kiongozi wa chama cha Labour, Jeremy Corbyn, amesema kuwa ni haki kwake kujiuzulu na kusisitiza kuwa  ni wakati sasa wa wananchi wa nchi hiyo kuamua mustakabali wa taifa lao kupitia uchaguzi mkuu wa haraka.

HABARI ZAIDI

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu