Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Toeni maoni ya kuboresha mitaala- Prof. Ndalichako

Ijumaa , 18th Jun , 2021

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako, ametoa wito kwa wadau wa elimu waliojitokeza katika mkutano wa kupokea maoni ya kuboresha mitaala nchini, kutoa maoni yatakayojikita kuwajengea wahitimu ujuzi na stadi zitakazoweshe kujitegemea.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako

Akizungumza katika mkutano huo uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam Prof. Ndalichako amesema ni matarajio kuwa maoni yatakayopatikana kutoka kwa wadau mbalimbali yatasaidia kujibu changamoto ya wahitimu kumaliza kisha kusubiria matangazo ya kazi badala ya kujiajiri wenyewe.

"Wadau wamekuwa na wito kuwa na mitaala ya kuwaandaa vijana kujitegemea kujiajairi au kuajiriwa, ni imani yangu kuwa kupitia mkutano huu mtatoa maoni na mapendekezo yanayolenga kujibu changamoto hii pia suala hili tuliwekee mkazo kwa sababu ni kilo cha wadau kuwa wahitimu wanamaliza wanasubiri tu matangazo ya kazi," amesema Prof. Ndalichako.

Awali akizungumza Prof. Ndalichako amesema serikali imejikita katika kujenga uchumi wa viwanda hivyo kuna budi kuwa na wahitimu wabunifu watakosaidi kukuza uchumi wa nchi.

"Tumejikita katika kujenga uchumi wa viwanda, lazima tuzalishe wahitimu wabunifu wa waweze kubuni vyanzo zaidi vya kukuza na kuimarisha uchumi wa taifa, taifa lisilo na wahitimu mahiri kamwe haliwezi kusonga mbele," amesema Prof. Ndalichako.

Aidha, Prof. Ndalichako amaeto wito kwa taasisi za elimu ya juu nchini kuendesha mijadala ya kupitia mitaala kwani itawasaidia kukusanya maoni na kuyafanyia maboresho.

"Nitoe wito kwa taasisi za elimu ya juu nchini waanzishe mijadala kama hii, na kupata maoni kwa wadau mjielekeeze kushirikiana na taasisi binafsi muweze kujua mataraijio ya wahatimu ili nanyi kuingia kazini kutazama kwa kina," amesema Prof Ndalichako.

Leo Prof. Ndalichako alikuwa mgeni rasmi katika mkutano wa kupokea maoni ya wadau kuhusu uboreshaji wa mitaala ya elimu ya awali, msingi na sekondari ulioandaliwa na Taasisi ya Elimu Tanzania nchini (TET).
 

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa