Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Tume ya ushirika yatishia kuvifuta vyama 1,862

Ijumaa , 20th Mei , 2016

Tume ya Maendeleo ya Ushirika inakusudia kuvifuta katika daftari la vyama vya Ushirika vyama ambavyo vimekiuka matakwa ya Sheria ya Vyama vya Ushirika Na.6 ya mwaka 2013.

Dk. Audax Rutabanzibwa, Kaimu Mrajis wa Vyama vya Ushirika

Kwa mujibu wa sheria, Mrajis wa Vyama vya Ushirika, kwa mamlaka aliyopewa chini ya vifungu Namba 11(3), 8(2) na 100 anatakiwa kuvifuta vyama ambavyo vimeshindwa kufanya kazi katika kutimiza masharti ya usajili wake.

Masharti yaliyokiukwa ni pamoja na kutokufanya Mikutano kwa mujibu wa Sheria, kutokufanya chaguzi za viongozi kwa mujibu wa Sheria, kuwa na Idadi pungufu yawanachama na kushindwa kufanya shughuli zake kwa zaidi ya miezi sita, kinyumena matakwa ya Sheria na masharti ya vyama hivyo.

Kutokana na sababu hizo, vyama vinavyokusudiwa kufutwa ni 1,862 na vitafutwa baada ya siku tisini (90) kuanzia tarehe 13 Mei, 2016 siku ambayo Tangazo la Kusudio la Kufuta vyama hivyo lilipochapishwa katika gazeti la Serikali.

Idadi ya vyama vinavyokusudiwa kufutwa katika kila mkoa ni kama ifuatavyo: Arusha vyama 83, Dar es Salaam 91, Dodoma 50, Geita 16, Iringa 74, Kagera 240, Katavi 19, Kigoma 38, Manyara 73, Mara 203, Morogoro 278, Mtwara 52, Njombe 18, Pwani 324, Rukwa 14, Ruvuma 14, Shinyanga 89, Simiyu 93, Singida 15, Tanga 77 na Lindi 1.

Orodha ya vyama vinavyokusudiwa kufutwa inapatikana katika Ofisi za Ushirika za Wilaya na Mikoa na katika tovuti la Tume ya Maendeleo ya Ushirika (www.ushirika.go.tz ) .

Mtu yeyote au Taasisi yenye pingamizi la msingi dhidi ya kufutwa kwa chama husika, anatakiwa awasilishe pingamizi hilo na sababu zake katika Ofisi ya Mrajisikupitia Ofisi za Warajis Wasaidizi wa Mikoa husika ndani ya siku tisini (90) kuanzia tarehe 13/05/2016, siku ambayo tangazo la kufutwa kwa vyama hivyo lilipotangazwa katika gazeti la Serikali.

Umma unataarifiwa kwamba zoezi la kufuta Vyama vya Ushirika ambavyo haviendeshwi kwa mujibu wa Sheria ni endelevu na kwa ajili hiyo viongozi na wanachama wa vyama vya Ushirika na Maafisa Ushirika wanaagizwa kuhakikisha kwamba Vyama vya Ushirika katika maeneo yao viendeshwe kwa kuzingatia matakwa ya Sheria ya Vyama vya Ushirika ili kuepuka vyama vyao kufutwa.

HABARI ZAIDI

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ