Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Tundu Lissu aikataa nafasi ya U-makamu wa rais

Alhamisi , 14th Mar , 2019

Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Antiphas Lissu amesema hana mpango wa kuchaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa nchi, hivyo anastahili kuendelea kupatiwa stahiki zake za ubunge zikiwepo posho na mshahara.

Mbunge Tundu Lissu

Lissu amesema hana mpango wa kuchaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa nchi, hivyo anastahili kuendelea kupatiwa stahiki zake za ubunge zikiwepo posho na mshahara.

Lissu aemeyasema hayo wakati akielezea vifungu vya sheria vilivyopo katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwamba katika Ibara ya 71, moja ya jambo ambalo litamfanya Mbunge kukoma kupatiwa stahiki zake ni pale anapoteuliwa au kuchaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa nchi.

Jana Februari 13,  Lissu amethibitisha kuwa uongozi wa Bunge kupitia kwa spika, Job Ndugai na katibu wake Steven Kagaigai umemfutia rasmi mshahara na posho za kibunge kwa kile alichoeleza kuwa ofisi ya spika haina taarifa za anachokifanya nje ya nchi.

"Katika Katiba ya nchi, Ibara ya 71 kati ya sababu zilizotajwa na ibara hiyo, sababu ya sita inasema endapo ukiteuliwa au kuchaguliwa kuwa Makamu wa rais, hutapata stahiki za kibunge. Mimi sitajii kuteuliwa au kuchaguliwa kuwa Makamu wa Rais", amesema.

Pamoja na sababu mbalimbali alizozitaja Mbunge huyo zitakazopelekea kunyimwa stahiki zake za Kibunge amesema hakuna sababu yoyote inayomfunga hivyo Bunge linapaswa kumpatia stahiki zake kwani kama ni kutokuwepo kwake bungeni, Spika Ndugai alikuwepo katika kikao kilichoadhimia yeye apelekwe Nairobi kwa matibabu wakati alipokuwa hoi baada ya kupigwa risasi Septemba 07, 2017.

Mbali na hayo Lissu amesema ameshawasiliana na wanasheria wake walipo Tanzania waweze kufungu mashtaka dhidi ya Bunge kwa kuzuia mishahara na posho zake.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava