
Askofu mstaafu Boniface Kwangu, aliyefariki dunia
Kauli hiyo imetolewa na Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Mhimbo Mndolwa, wakati mwili wa Askofu Mstaafu Kwangu ukiagwa ndipo akaomba uchunguzi wa kina ufanyike ili kuwababini waliofanya mauaji hayo ya kutisha
"Tunaiachia serikali kwa wahusika wa kifo cha Askofu Mstaafu Kwangu kama kuna aliyehusika basi sheria ichukue mkondo wake," amesema Askofu Mndolwa
Akisoma risala ya marehemu Askofu Mstaafu Kwangu, Benedict Kwangu, amelishukuru jeshi la polisi kwa kushirikiana na wavuvi wa eneo hilo kuweza kufanikisha kuupata mwili wa Askofu huyo.