Alhamisi , 11th Jul , 2019

Baraza la Mitihani la Taifa limetoa pongezi kwa walimu, Maafisa elimu kwa kusimamia vizuri kazi ya ufundishaji na  kufanikisha kwa kiasi kikubwa, shule zote nchini kufanya vizuri, ambapo ufaulu umeongezeka, kutoka asilimia 97.58 mwaka 2018, hadi kufikia asilimia 98.32 mwaka 2019.

Katibu Mtendaji wa NECTA Dkt Charles Msonde.

Akitoa taarifa ya matokeo hayo Mjini Unguja, Katibu Mtendaji wa Baraza hilo Dkt Charles Msonde, amesema kuwa jumla ya watahiniwa 88,069 sawa na asilimia 98.32, ya watahiniwa wote waliofanya mtihani wamefaulu.

Kwa mujibu wa Dkt Msonde watahiniwa 91,298 walisajiliwa wakiwamo wasichana 37,948 sawa na asilimia 41.56 na wavulana 53,350 sawa na asilimia 58.44. ambapo kati ya watahiniwa waliosajiliwa, watahiniwa wa shule walikuwa 80,216 na watahiniwa wa kujitegemea walikuwa ni 11,082.

Aidha watahiniwa 91,298 waliosajiliwa kufanya mtihani, watahaniwa 90,001, sawa na asilimia 98.58 walifanya mtihani, na wataniwa 1297 sawa na asilimia 1.42 hawakufanya mtihani huo kulingana na sababu mbalimbali ikiweme ugonjwa na utoro.

Dkt Msonde ameongeza kuwa, watahiniwa wa shule kati ya watahiniwa 80,216 waliosajiliwa , watahiniwa 79,770 sawa na asilimia 99.44, walifanya mtihani, ambapo wasichana walikuwa 33,883 sawa na asilimia 99.57, na wavulana 45,887 sawa na asilimia 99.35, ambapo watahiwa 446 sawa na asilimia 0.56 hawakufanya.

Ambapo watahiniwa wa kujitegemea kati ya 11,082 waliosajiliwa, 10, 231 sawa na asilimia 92.32 walifanya mtihani, na watahainiwa 851 sawa na asilimia 7.68 hawakufanya.