Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ujue undani wa Madereva waliokutwa na Corona Kenya

Jumatano , 20th Mei , 2020

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema kuwa, amebaini kuwa kitendo cha Serikali ya Kenya kuwapima Madereva 19 Watanzania na kuwakuta na maambukizi ya Virusi vya Corona ni njama za kuua soko la utalii nchini, kwani baada ya madereva hao kupimwa hapa nchini walikutwa hawana Virusi.

Malori ya Mafuta

Mrisho Gambo ameyabainisha hayo leo Mei 20, 2020, kupitia taarifa yake kwa Vyombo vya Habari na kueleza ni hatua zipi ambazo wamezichukua baada ya kubainika uwepo wa wimbi kubwa la maambukizi ya Virusi vya Corona mipakani, na kusema kuwa hata wao wameanza kuwapima Madereva wanaotoka nchi hiyo jirani kupitia mpaka wa Namanga na wengi wao wana maambukizi.

"Ili kujiridhisha upya tulichukua tena Sampuli za Madereva 19, waliopimwa Namanga upande wa Kenya na kukutwa wana maambukizi, Sampuli hizi tuzipeleka Maabara Kuu ya Taifa Dar es Salaam, majibu yalionesha kuwa madereva hao hawana maambukizi ya Virusi vya Corona, Mkoa umejiridhaisha kwamba hizi ni mbinu za nchi ya Kenya kuua soko la utalii nchini" imeeleza taarifa ya RC Gambo.

Aidha RC Gambo amesema kuwa jumla ya Sampuli 67 za madereva wanaotoka Kenya zimekwishapimwa, "Madereva 44 kutoka Kenya walichukuliwa vipimo Mei 14 na majibu yalitoka Mei 16 na  kati ya hao madereva 14 walikutwa na Corona, kati ya hao Wakenya ni 11, Mganda 1 na 2 nchi tumeihifadhi, aidha Mei 16 walipimwa madereva 23 kutoka Kenya, na majibu yalitoka Mei 18, ambapo kati ya hao 10 walikutwa na maambukizi na wote ni raia wa Kenya". 
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali