Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ukarabati kituo cha umeme Kipawa karibu kukamilika

Jumapili , 31st Aug , 2014

Kazi ya ukarabati wa kituo kikubwa cha kusambazia umeme cha Kipawa ambacho kilipata hitilafu na kuharibika juzi saa Saba usiku inaelekea kukamilika baada ya maeneo mengi yaliyoathiriwa na hitilafu hiyo kuanza kupata umeme.

Meneja wa Tanesco Mkoa wa Ilala, Mhandisi Atanasius Nangali.

Meneja wa Tanesco mkoa wa Ilala mhandisi Atanasius Nangali, ameiambia East Africa Radio kuwa kazi ya ukarabati inaendelea vizuri ambapo mafundi wa shirika hilo wamekuwa wakifanya kazi usiku na mchana kuhakikisha umeme unarejea.

Ameyataja maeneo ambayo bado umeme haujarejea mpaka sasa kuwa ni Gongolamboto, Kivule na Kipunguni na kwamba muda wowote kuanzia sasa umeme katika maeneo hayo utarudi katika hali yake ya kawaida.

Kwa mujibu wa mhandisi Nangali, hitilafu hiyo ilisababisha maeneo mengi ya wilaya za Temeke, Ilala na Kisarawe kukosa nishati ya umeme, na kwamba juhudi zilifanyika za kurejesha umeme katika maeneo nyeti ikiwa ni pamoja na uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere ambako mafundi wa TANESCO mkoa wa Ilala waliandaa njia ya moja kwa moja ya umeme kutoka maeneo mengine ya jiji kuelekea uwanjani hapo.

Aidha, mhandisi Nangali amesema hitilafu hiyo ni ya kiufundi na kuongeza kuwa matukio ya aina hiyo yamekuwa nadra hivi sasa kwani shirika limeimarisha ukarabati wa miundombinu yake ikiwa ni pamoja na njia zilizochakaa pamoja na mifumo ya usambazaji.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya