Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

UKAWA waanza mbio zao, elimu kipaumbele cha kwanza

Jumamosi , 29th Aug , 2015

Chama Cha Demokrasi na Maendeleo kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) leo kimezindua rasmi kampeni za urais ambapo uzinduzi huo umeshuhudia umati wa watu wakijitokeza.

Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA akiwakilisha Umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA, Mh. Edward Lowassa

Akiongea katika mkutano huo Mgombea urais kupitia Umoja huo Mh. Edward Lowassa amesema kuwa wananchi watakapompa ridhaa ya kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano ataendesha mchakamchaka wa mabadiliko katika sekta zote.

Mh. Lowassa amesema kuwa ataweka vipaumbele katika sekta ya viwanda pamoja na kuboresha sera ya elimu ambayo ndio chachu ya mabadiliko katika kujenga uchumi wa nchi yoyote duniani.

Kwa upande wake mgombea mwenza Juma Duni Haji amesema kuwa watanzania wametaabika kwa muda mrefu bila kupata utatuzi wa matatizo yao ikiwemo maisha bora ila kwa serikali itakayoundwa na Mh. Lowassa itajenga mazingira bora kwa kila mtanzania.

Naye waziri mkuu mstaafu wa awamu ya tatu Mh. Fredrick Sumaye amesema kuwa ufisadi unaofanyika ndani ya Chama cha Mapinduzi ni mkubwa na wao kwa nafasi zao walikuwa wanashindwa kufanya maamuzi kutokana na mfumo uliokuwepo ndani ya chama hicho.

Aidha Mh. Sumaye amefafanua kashfa zinazotokea nchini Tanzania nyingine ni mpango wa kutengeneza kuwachafua baadhi ya watu kwa kuwa chama hicho kina mgawanyiko mkubwa ambapo watu wenye msimamo wanachafuliwa ili wasipate nafasi.

Kwa upande wake mwenyekiti wa CHADEMA Mh. Freeman Mbowe amesema kuwa wamemchagua lowassa kuongoza mabadiliko kwa kuwa ni mtu ambae anauwezo wa kuamua na kuwatumikia wananchi.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali