
Vijana wa kitanzania katika shughuli zao
Mtaalam wa ajira kwa vijana kutoka Shirika la Kazi Duniani, ILO, Bi. Annamarie Kiaga, amesema, kutowashirikisha vijana kutachelewesha maendeleo yao na taifa kwa ujumla hivyo ni vyema ikaundwa sera ya namna ya kuwashirikisha na kujitegemea.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Michezo na Sanaa, Profesa Elisante Ole Gabriel, amesema ni vyema vijana wakajenga tabia na mitazamo ya kujitegemea ki-fikra bila kusukumwa kwani serikali inathamini mchango wao katika kuleta mabadiliko chanya baina yao na jamii kwa jumla.