Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Vitambulisho vyachanganya wafanyabiashara

Alhamisi , 14th Feb , 2019

Suala la ugawaji wa vitambulisho vya wajasiriamali wadogowadogo limeendelea kuzua sintofahamu na changamoto nyingi katika mikoa mbalimbali nchini kutokana na maelezo tofauti tofauti yanayotolewa.

Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi (kushoto) akikabidhi vitambulisho vya wajasiriamali wadogowadogo

Baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli kugawa vitambulisho vya awamu ya kwanza, Desemba 10, 2018 kwa wakuu wa mikoa, ugawaji wake ulionekana kwenda kwa kusuasua na hilo lilithibitishwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi, Januari 28, 2019 alipokuwa akigawa vitambulisho hivyo kwa awamu ya pili kwa wakuu wa mikoa.

Kwa mujibu wa Rais Magufuli, wakati akigawa vitambulisho vya wajasiriamali awamu ya kwanza alisema kuwa vitagawiwa kwa wajasiriamali wadogowadogo ambao mitaji yao haiziadi sh. Milioni 4.

"Mfanyabiashara mdogo mwenye mtaji chini ya Shilingi milioni 4 akiwa na kitambulisho hiki sitaki TRA, Halmashauri wala Mgambo kuwasumbua. Nawapa tu onyo msije mkachukua bidhaa za wafanyabiashara wakubwa mkawa mnawauzia ili wakwepe kodi".

"Kitambulisho kimoja ni Sh. 20,000/= hivyo kwa vitambulisho 25,000 itakuwa jumla ya Sh. 500,000,000/= na ipelekwe TRA ili wasije sema ni mradi wangu wakati mimi ni facilitator tu. Waambieni wasaidizi wenu wasiviuze kwa bei zaidi ya hii iliyopangwa", alisema Rais Magufuli.

Wakati huohuo Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji hivi karibuni amewataka wajasiriamali wadogowadogo ambao mauzo yao hayavuki sh. Millioni 4 kwa mwaka kuchamgamkia fursa hiyo ili wasibughudhiwe.

Mtazamo wa kauli ya Naibu Waziri inaonesha kutofautiana na maagizo ya Rais Magufuli ambayo aliyatoa wakati akigawa vitambulisho vya awamu ya kwanza, na hicho ndicho ambacho wajasiriamali wengi wadogowadogo wamekuwa wakikilalamikia.

Baadhi ya wafanyabiashara wa mkoani Tabora wamemlalamikia Mkuu wa Mkoa huo, Aggrey Mwanri kuwa kutokana na wafanyabiashara kutokuwa na mahesabu ya kiasi gani wanaingiza kwa mwaka na biashara nyingi kuwa za msimu na zenye faida ndogo, wanashindwa kumudu gharama ya sh. 20,000 kwa kila kitambulisho.
 

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa