Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wachepushaji wa maji waendelea kusakwa

Alhamisi , 22nd Sep , 2022

Timu ya Wataalam kutoka Bodi ya Maji Bonde la Wami/Ruvu imeendelea kufanya ukaguzi wa matumizi ya maji kutoka maeneo mbalimbali ya vyanzo vya maji. 

Timu ya Wataalam waliopo zone ya Mto Lukulunge na Ngerenge imefanikiwa kubaini mifereji zaidi ya mitatu na kuifunga yote kwa pamoja upande wa juu wa Mto Lukulunge ambayo ilikuwa imebadilisha uelekeo na kupunguza wingi wa maji mtoni. 

Timu hiyo ya wataalam imebaini uvunaji wa maji kwa kutumia Pump unaofanywa na askari kikosi cha jeshi la Wananchi. Pump hiyo imekabidhiwa kwa Mkuu wa kikosi cha Mbinga na kupewa elimu ya usimamizi wa Rasilimali za maji ili iwe mfano kwa sehemu ya watumiaji wa Maji. 


Kutoka zone ya Ruvu Chini timu ya wataalam wa bonde la Wami/Ruvu imefanikiwa kubaini uchepushwaji wa Maji kutoka Mto Ruvu unaofanywa na mwekezaji wa mabwawa ya samaki anayefahamika kwa jina la ndugu Eliona Koka wa kijiji cha Kisabi kata ya Muungano halmashauri ya  Kibaha. 

Katika ukaguzi huo timu ya wataalam wa Bonde la Wami wakiambatana na Wataalam wa Mamlaka ya Maji Dawasa wamefanikiwa kubaini matumizi ya maji isivyo halali kinyume na Sheria ya rasilimali za Maji ya Mwaka 2009.

Mmiliki huyo amekutwa akiendesha shughuli za ufugaji wa samaki katika vizimba huku akiwa hana vibali vya matumizi ya maji kutoka mtoni jambo linalopelekea kuvunja sheria ya usimamizi wa rasilimali za maji. 

Lengo la Ukaguzi huo ni kufanya tathimini ya maji pamoja na kutoe elimu ya urasimishaji wa matumizi na utunzaji wa rasilimali za maji

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi