Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wafuasi 30 wa CUF wafikishwa mahakamani

Alhamisi , 29th Jan , 2015

Wafuasi 30 wa chama cha wananchi (CUF) leo wamefikishwa mahakamani baada ya kukamatwa na polisi juzi wakiwa katika maandamano kuadhimisha mauaji ya wenzao yaliyotokea mwaka 2001 visiwani Zanzibar.

Wafuasi 30 wa chama cha wananchi (CUF) akiwemo Naibu Mkurugenzi wa Oganaizesheni, Uchaguzi na Bunge Shaweji Mketo na mkurugenzi wa mawasiliano Abdul Kambaya wamefikishwa mahakamani kwa tuhuma za mashitaka matatu likiwemo la kufanya mkusanyiko usio halali, ambapo wameshindwa kutimiza masharti na dhamana na kupelekwa rumande.

Wakili wa serikali Joseph Maugo amedai mbele ya hakimu Emilius Mchauro wa mahakama ya hakimu mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam kuwa washtakiwa wanatuhumiwaa kwa mashtaka matatu ambapo shitaka la kwanza linalowakabili washtakiwa wote ambao wanatuhumiwa kula njama ya kufanya uhalifu.

Shitaka la pili linawakabili washtakiwa 28 ambao wanatuhumiwa kufanya mkusanyiko usio halali.
 
Imedaiwa kuwa walifanya mkusanyiko huo Januari 27 mwaka huu, wakiwa katika ofisi ya CUF iliyopo karibu na hospitali ya Temeke bila uhalali wowote walifanya mkusanyiko kwa nia ya kufanya maandamano kuelekea viwanja vya Zakhiem, Mbagala, Dar es Salaam.
 
Katika shitaka la tatu pia linawakabili washtakiwa 28, wanadaiwa kufanya mgomo baada ya katazo halali ambapo washtakiwa bila kujali tangazo lililotolewa na jeshi la polisi la kutokufanya maandamano wao walikaidi.

Washitakiwa wote wamekana kuhusika na tukio hilo huku wakili Maugo akidai upelelezi bado na pia kisheria mashitaka yao yana dhamana.

Mchauro amesema ili washtakiwa wawe nje kwa dhamana wanatakiwa wasaini dhamana ya sh. 100,000 na mdhamini mmoja wa kuaminika, lakini washtakiwa walishindwa kutimiza masharti ya dhamana na kurudishwa rumande.
 
Washtakiwa hao watarudishwa mahakamani Januari 30 ili kuangalia kama wametimiza masharti ya dhamana, baada ya barua za wadhamini kwenda kuhakikiwa na upande wa mashtaka.
 
Nje ya mahakama hiyo kundi la wafuasi wa chama hicho walionekana wakihangaika huku na kule wakitaka kuwadhamini ndugu zao bila mafanikio na baada ya zoezi hilo kukwama walisubiri kuona wafuasi hao wanavyoondoka mahakamani hapo ambapo waliwasindikiza kwa nyimbo za chama hicho.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa