Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Wagonjwa wa Corona walitaka kutoroka" - DC Ilala

Alhamisi , 23rd Apr , 2020

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema, amesema kuwa bado hajapata taarifa za waathirika wa Virusi vya Corona, waliopo katika kituo maalum katika Hospitali ya Amana, kama wametoroka na kurejea makwao ila anachojua walikuwa wanatishia kuondoka kwa madai ya kuwa hali zao kiafya ni nzuri.

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema.

Mjema ameyabainisha hayo leo Aprili 23,2020, wakati akizungumza na ITV, kufuatia taarifa mbalimbali zilizokuwa zikisambaa kwenye mitandao ya kijamii zikieleza kuwa, baadhi ya wagonjwa katika hospitali hiyo wameleta vurugu na wengine kutoroka.

"Bado hatuna taarifa ya wagonjwa katika Hospitali ya Amana waliotoroka na kupanda daladala kurejea makwao, ngoja tuifuatilie ila tunachojua ni kwamba walikuwa wanasema wanataka kurudi nyumbani, kifupi walikuwa wanatishia tu" DC Ilala, Sophia Mjema.

Aidha DC Mjema ameongeza kuwa "Kulikuwa na wagonjwa ambao walikuwa wamefika pale na kusema kuwa wao hawaumwi sana kwahiyo walikuwa wanataka waruhusiwe na unajua ukifika pale, ukiwa mshukiwa lazima ukae kidogo hospitali uangaliwe wakuone upo vizuri ndiyo uruhusiwe".

EATV&EA Radio Digital, ilimtafuta Mkuu huyo wa Wilaya kwa ajili ya kupanda undani wa taarifa hizo, ambapo alidai kuwa yupo kwenye kikao na akitoka basi atatupigia simu na kutueleza ni kipi kilichojiri na hatua zipi ambazo zimekwishachukuliwa hadi sasa.
 

HABARI ZAIDI

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi