
Mkuu wa mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani,
Akizungumza katika hafla fupi ya utiaji saini wa mikataba hiyo amesema, kufanya hivyo ni mkakati wa serikali nchini katika kukabiliana na tatizo la lishe duni kwa wananchi wake ikiwemo watoto na akinamama wajawazito.
Aidha amesema tatizo la udumavu wa watoto kwa Mkoa wa Tabora kutokana na lishe duni lipo kwa 25% ambapo katika hafla hiyo amewaagiza wakuu wa wilaya kuhakikisha wanakwenda kusimamia vyema shughuli zote za kuimarisha lishe kwa wananchi.
Aidha amewaambia wakurugenzi watendaji wa halmashauri kuendelea kutenga fedha za lishe pamoja na kwenda kutumika kama ambavyo serikali imekusudia kuimarisha lishe kwa wananchi wake na si kutumika vinginevyo.