Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Walioiba mafuta ya SGR wahukumiwa

Alhamisi , 26th Jan , 2023

Mahakama ya wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza imewahukumu kwenda jela miaka miwili au kulipa faini washtakiwa watatu kati ya sita waliohusika na wizi wa mafuta ya petroli yaliyokuwa yanatumika katika ujenzi wa reli ya kisasa SGR 

Akisoma hukumu hiyo hakimu mkazi mwandamizi wa mahakama hiyo John Jagadi amesema washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka matatu yakiwemo ya kupatikana na mali ya wizi, kufanya biashara ya mafuta bila kuwa na leseni pamoja na kufanya biashara ya mafuta ya petroli katika mazingira hatarishi ambapo washtakiwa hao walikiri makosa mawili 

Katika kesi namba 15 inayomkabili Levy Daniel na Fredy Magay ambao walikamatwa mnamo tarehe 23 na mafuta ya petroli lita nne na wakakiri kosa moja kufanya biashara ya mafuta bila kuwa na leseni

Katika shtaka la kufanya biashara bila kuwa na leseni hakimu Jagadi amesema kwa mujibu wa kifungu namba 132 kifungu kidogo cha kwanza na cha nne cha sheria ya udhibiti wa nishati washtakiwa hao watatakiwa kutumikia kifungo gerezani cha miaka miwili au kulipa faini ya shilingi laki moja kila mtu

Aidha katika kesi nyingine namba 9 ya mwaka huu inayomkabili Dotto Ihanu ambae amekiri kufanya biashara ya mafuta bila kuwa na leseni pamoja na kuuza mafuta ya petroli katika mazingira hatarishi ambapo mnamo tarehe 23 ya mwaka huu wilayani Kwimba alikamatwa na lita 21 za mafuta ya petrol

Katika shtaka la kufanya biashara bila kuwa na leseni mahakama hiyo imemhukumu kifungo cha miaka miwili gerezani au kulipa faini ya shilingi laki moja na elfu hamsini huku katika shtaka lingine la kufanya biashara ya mafuta katika mazingira hatarishi akihukumiwa kwenda gerezani miezi sita au kulipa faini ya shilingi laki moja

Mahakama imesema washtakiwa wote watatu kama wakifanikwa kulipa faini shtaka moja la kupatikana na mali ya wizi lina dhamana na wakikidhi masharti ya dhamana watakuwa huru huku kesi hiyo ikipangwa tena hadi tarehe 9 ya mwezi wa pili mwaka huu.
 

HABARI ZAIDI

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea