Vyoo vya shule ya msingi Kasaba vilivyotitia na kulia ni baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo
Wakielezea adha hiyo wanafunzi wamesema kwanza hawana maji wala vyoo kwani vilititia na shule ilichimba mashimo machache ya muda ili yawasitiri ambayo hata hivyo asilimia kubwa hawayatumii kwa kuhofia usalama wake kwani yamekuwa yakibomoka mara kwa mara.
Aidha, wanafunzi hao wameongeza kuwa shule hiyo pia inakabiliwa na upungufu wa madarasa ambayo hulazimisha wanafunzi kurundikana huku kukiwa na vyumba vilivyojengwa kwa nguvu za wananchi ambavyo hadi sasa havijakamilishwa.

