Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wananchi wameteseka tangu dunia iumbwe- Magufuli

Ijumaa , 21st Jul , 2017

Rais Magufuli ameitaka kampuni ya Nyanza inayoshughulikia ujenzi wa barabara ya mkoani Kigoma kuanza kufanya kazi usiku na mchana kwa kuwa wapo baadhi ya wananchi hawajahi kuona lami maisha yao yote mpaka wanakufa.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo wakati akihutubia wakazi wa Kakonko mkoani Kigoma katika uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Kibondo mpaka Nyakanazi yenye urefu wa kilomita 50 kwa kiwango cha lami.

"Wananchi hawa wanahitaji barabara ya lami wameteseka tangu dunia iumbwe, wako watu hawajui rangi ya lami, wapo watu hapa wamezaliwa, wamezeeka hawajui rangi ya lami ikoje. Kwa sababu hawajawahi kuona barabara ya lami katika maisha yao, kwa hiyo nataka hii lami ianze na mjipange kweli mfanye kazi usiku na mchana", amesema Rais Magufuli. 

Pamoja na hayo Rais Magufuli amewaagiza makandarasi kufanya kazi ipasavyo na wasipofanya hivyo watachukuliwa adhabu kali zidi yao.

"Kwa bahati nzuri mimi kufukuza makandarasi ni kama kunywa chai, sasa asije akanirudisha kule nilipokuwa kwa sababu sasa ni Baba wa wote lakini nilipokuwa Waziri nilikuwa nafukuza tu, kwa kupitia bodi ya makandarasi nilikuwa nafuta wakandarasi na mimi nikuombe Prof. Mbalawa usiwe mpole. Makandarasi watakao kuwa wanafanya kazi hovyo hovyo, pole pole chukua 'action' ili kusudi kama kashindwa kufanya kazi ya ukandarasi akafanye nyingine hata ya kuvua samaki", amesisitiza Rais Magufuli.

Kwa upande mwingine, Rais Magufuli amewataka wananchi kibondo na kasuru wa mkoa wa Kigoma na watanzania wote kwa ujumla kudumisha ulinzi na usalama katika maeneo yao wanayoishi ili kupunguza au kumaliza kabisa matatizo ya kihalifu yanayotokea.

HABARI ZAIDI

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani