Ijumaa , 20th Aug , 2021

Polisi wilayani Moroto Kaskazini mwa Uganda, wameanza kuwakamata watu wanaonunua chapati tano au zaidi kwa madai ya kwamba huenda wanawalisha wezi wa mifugo katika eneo hilo.

Chapati

Akizungumza na kituo cha Radio cha Uganda Network, Msemaji wa Polisi wa mkoa wa Karamoja, Michael Longole, amesema kwamba hatua hiyo imekuja baada ya kubaini kwamba watu wengine hununua chapati zaidi ya tano na kuwapelekea wezi waliojificha vichakani baada ya kukimbia makazi yao.

Aidha, Longole alisisitiza kwamba huenda kwa kufanya hivyo kutawalazimu wezi hao kutoka mafichoni na kusalimisha silaha walizonazo.