Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wanasiasa wamlilia mfanyabiashara Ali Mufuruki

Jumapili , 8th Dec , 2019

Mbunge wa Kigoma Mjini, na kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, ameonesha kupokea kwa masikitiko makubwa kufuatia kifo cha Mfanyabiashara maarufu hapa nchini, Ali Mufuruki, aliyefariki Dunia akiwa nchini Afrika ya Kusini.

Aliyekuwa Mfanyabiashara maarufu Tanzania, Ali Mufuruki.

Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Kijamii wa Twitter, leo Desemba 8, 2019, Zitto, ameandika maneno yaliyoonesha ni kwa namna gani, alikuwa akimfahamu mfanyabiashara huyo.

"Sina maneno ya kusema zaidi ya kuwa sote ni wake Mwenyezi Mungu na kwake sote tutarejea, sio tu alikuwa rafiki bali alikuwa mshauri wangu, tulipishana mawazo fulani lakini alikuwa na heshima kubwa, tangulia ndugu yangu RIPMufuruki" ameandika Mbunge Zitto Kabwe.

Mwanasiasa mwingine aliyeonesha kuguswa na msiba wa Ali Mufuruki ni mwanasiasa wa muda mrefu Khamis Kagasheki, ambaye ameandika hivi.

"Kwa mshtuko na masikitiko nimepata taarifa kwa kifo cha Ndg Ali Mufuruki, pigo kubwa kuondokewa na Ali, mkono wa pole nyingi kwa familia yake, MwenyeziMungu amhurumie na amsamehe. Ali you will be missed immensely".

Wengine walioguswa na kutuma salamu za pole kwa ndugu jamaa na marafiki wa mfanyabiashara huyo ni pamoja na Ubalozi wa Ujerumani hapa nchini Tanzania.

Ali Mfuruki aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Vodacom Tanzania, aliyehudumu kwa muda wa miaka miwili, ambapo baadaye alitangaza kujiuzulu nyadhifa zake zote kuanzia Desemba 1, 2019.
 

HABARI ZAIDI

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma

Mkuu wa Usalama Barabarani mkoa wa Songwe Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Charles Bukombe, akizungumza na abiria

"Fungeni mikanda muda wapo safarini" - SSP

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri