Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wanawake waiteka sekta ya Uvuvi na kilimo Afrika

Alhamisi , 21st Mar , 2024

Wanawake wachakataji na wafanyabiashara wa mazao ya uvuvi barani Afrika wametajwa kuwa na mchango mkubwa katika Sekta ya Uvuvi hususan katika uchatakaji na kilimo cha mwani.

Afisa Uvuvi Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Jovice

Afisa Uvuvi Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Jovice Mkuchu amebainisha hayo Machi 21, 2024 jijini Dar es salaam wakati akifungua kikao cha mtandao wa wanawake barani Afrika wanaochakata mazao ya uvuvi kilicholenga kukuza uelewa wa uongozi katika nchi zao.

Aidha Bi. Mkuchu amesema, serikali inatambua umuhimu wa wanawake katika kuwezesha na kuendeleza Sekta ya Uvuvi barani Afrika, ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekuwa akiwezesha na kuinua wanawake kwenye kilimo cha mwani na shughuli za uvuvi.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Mtandao wa Wanawake Afrika Wanaojishughulisha na Uchakataji na Biashara ya Samaki (AWFISHNET) wenye makao makuu nchini Tanzania Bi. Editrudith Lukanga, amebainisha kuwa mtandao huo una wanawake ambao ni viongozi wa mtandao kutoka nchi mbalimbali takriban 44.

Bi. Lukanga amesema kuwa mtandao huo ulianzishwa Mwaka 2017 kwa msaada wa Umoja wa Afrika (AU) kupitia Shirika la Umoja wa Afrika la Rasilimali za Wanyama (AU-IBAR), ambapo katika kikao hiki kinachofanyika nchini moja ya malengo makuu ni kutafuta suluhu ya changamoto zinazowakabili wanawake katika Sekta ya Uvuvi.

Pia, amesema wanawake wanapaswa kushiriki kikamilifu katika kukuza Sekta ya Uvuvi kwa kuwa asilimia 60 ya wanaoshiriki katika mnyororo wa thamani baada ya samaki kuvuliwa ni wanawake.

Ameongeza kuwa mtandao huo unaangalia namna wanawake wanavyoweza kushiriki kikamilifu katika kutatua changamoto, kuangalia katiba na mpango mkakati kwa kuwa na sauti moja barani Afrika na kumfanya mwanamke aweze kuthaminika katika hali inayotakiwa.

Nao baadhi ya washiriki wa kikao hicho wamesema wamekuwa wakipata elimu na kubadilishana mawazo kutoka nchi mbalimbali barani Afrika ili mtandao huo uwe na tija katika kukuza Sekta ya Uvuvi.

Wamebainisha kuwa baadhi ya changamoto za Sekta ya Uvuvi barani Afrika zimekuwa zikifanana hivyo itakuwa rahisi kwao kuwa na sauti ya pamoja katika kupata suluhu ya changamoto hizo.
 

HABARI ZAIDI

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi