Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wanawake wawili wauawa kwa mapanga Geita

Ijumaa , 22nd Apr , 2016

Wanawake wawili akiwemo mhudumu wa afya wa zahanati ya Kagu iliyopo kijiji cha Kagu mkoani Geita wameuawa kwa kukatwa katwa kwa mapanga katika matukio mawili tofauti.

Wanawake wawili akiwemo mhudumu wa afya wa zahanati ya Kagu iliyopo kijiji cha Kagu Elizabeth Misango [54] na wa pili Helena Paulo [56] mkazi wa kijiji cha Luhuha mkoani Geita wameuawa kwa kukatwa katwa kwa mapanga ikiwemo kuchinjwa shingoni katika matukio mawili na maeneo tofauti usiku wa April 21.

Matukio hayo yamedaiwa kutokea katika mazingira yanayohusishwa na imani za kishirikina na tayari watu wawili wanaisaidia polisi katika upelelezi wa matukio hayo ambayo yameibua simanzi kubwa katika vijiji yalikotokea na viunga vya mji wa Geita.

Katika tukio la kwanza watu watatu wasiojulikana wakiwa na pikipiki walifika nyumbani kwa Elizabeth Misango karibu
saa mbili usiku katika kijiji cha Kagu na kumuamsha wa kudai wana mgonjwa lakini alipotoka nje na kujitambulisha walianza kumshambulia kwa kumkata kata kwa mapanga na kumchinja shingoni na alifariki palepale na wao kutoweka.

Kamanda wa polisi mkoa wa Geita Mponjoli Rodson amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kufafanua kuhusu mauaji ya Elizabeth Misango (Sikiliza sauti yake hapo chini)

Kwa upande wake Mganga mfawidhi wa Hospitali teule ya rufaa ya mkoa wa Geita Dkt Adam Sijaona amezumgumzia kifo cha mhudumu wa Afya Elizabeth Misango.

Katika tukio la pili Helena Paulo [56] akiwa njiani na mumewe Joseph Lubaga saa tatu na dakika 45 usiku katika kijiji cha Luhuha wakirejea nyumbani ghafla walivamiwa na watu wawili mmoja akiwa na panga na kuanza kumkatakata marehemu ambaye alifariki muda mfupi baadaye akiwa hospitalini akipatiwa matibabu.

Kamanda Mponjoli ameiomba jamii kubadilika na kuachana na imani potofu za kishirikina ambazo ndizo zimekuwa chanzo cha mauaji hayo ya kikatili.

Kwa upande wao Diwani Kulubone Pancrasi na Afisa mtendaji wa kata ya Kagu David Makanza wameapa kusaidiana na vyombo vya dola kuhakikisha waliohusika na mauaji hayo wanapatikana.

HABARI ZAIDI

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma

Mkuu wa Usalama Barabarani mkoa wa Songwe Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Charles Bukombe, akizungumza na abiria

"Fungeni mikanda muda wapo safarini" - SSP