Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Warioba afichua siri nzito siku ya uhuru

Jumamosi , 8th Dec , 2018

Waziri Mkuu wa 5 wa Tanzania, Joseph Warioba amefunguka juu ya tarehe 9 Disemba, siku ya ambayo Tanzania imekuwa ikisheherekea kupatikana kwa uhuru, ambapo ameeleza kwa wakati huo kuendesha nchi ilikuwa ni kitu kigumu sana kwa sababu kulikuwa na wasomi wachache.

Waziri Mkuu wa 5 wa Tanzania, Joseph Warioba.

Kwa mujibu wa Warioba ambaye kwa sasa ana miaka 78, wakati Tanganyika inapata uhuru yeye alikuwa na miaka 21 na kwa wakati huo nchi nzima ilikuwa na wahandisi wawili tu.

"Nakumbuka nilikuwa kijana wakati ule, na tulikuwa kwenye mapambano ya kupata uhuru, na tulishangazwa sana kuona bendera ya mkoloni inashushwa na bendera yetu ya Tanganyika inapanda, na baada ya hapo Mwalimu Nyerere alitushinikiza tufanye kazi kwa bidii." Amesema.

"Wakati tunapata uhuru kulikuwa na ubaguzi, waafrika tulikuwa tunaonekana ni watu wa hali ya chini, lakini siku hiyo tukaanza kujiona ni binadamu kama binadamu wengine." Ameongeza Warioba.

"Ni kweli wakati ule kulikuwa na wasomi wachache sana, mfano wahandisi nchi nzima walikuwa wawili tu na ukija kwenye taaluma nyingine walikuwa ni wachache tu japo mipango ilishaanza kuwepo ya kuwa na wasomi, ndiyo maana miezi miwili kabla ya uhuru kikafunguliwa chuo kikuu." Amesema.

Ameongeza kuwa kuhusu usafiri kipindi kile hali ilikuwa ngumu sana, ukilinganisha na sasa hivi, ambapo tumeendelea sana, kila kona kuna lami maeneo na yanafikika kwa urahisi.

Disemba 9, Tanzania inaadhimisha miaka 57 ya uhuru, ambapo Rais Magufuli licha ya kuwasihi watanzania kuendelea kufanya kazi pia aliamuru kiasi cha fedha kilichopangwa kutumika kwenye maadhimisho hayo kikatumike kujenga hospitali ya Uhuru Jijini Dodoma pamoja na kutangaza kuwasamehe wafungwa 1,076.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi