Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania Macrice Mbodo
Hayo yamebainishwa na Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania Macrice Mbodo, jijini Arusha, wakati wa mafunzo ya usalama kwa wakuu wa Idara za Usalama za Posta Afrika yanayofanyika jijini Arusha yakilenga kuwajengea uwezo na ubora katika utoaji huduma kwa njia ya teknolojia.
Matarajio ya mafunzo hayo ni kuona wataalamu wa Shirika la Posta Tanzania na Afrika wanaongezeka na kuendana na mabadiliko ya teknojolia ili kufanya kazi kwa weledi kwa kuzingatia usalama wa wateja.
Baada ya mafunzo haya siku tatu kutamatika na kufaulu yataiwezesha Tanzania kupata cheti cha uthibitisho cha kimatifa kuwa ni salama katika kutoa huduma za Posta.