Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Washindwa kusali baada ya kanisa kubadilishwa jina

Jumatatu , 5th Dec , 2022

Waumini wa kanisa la EAGT jimbo la Mwanza kusini wamekumbwa na taharuki baada ya kukuta kanisa lao limebadilishwa jina bila wao kujua hali iliyozua mzozo katika kanisa hilo na kusababisha shughuli zote za ibada kukwama

Wakizungumza na EATV viongozi wa kanisa hilo wamesema mgogoro huo uliibuka siku nne zilizopita lakini ghafla wakashangaa Jumapili wakakuta jina la kanisa hilo limebadilishwa na kuandikwa ASSEMBLIES OF GOD GOSPEL CHURCH INTERNATIONAL AGGCI na wakishindwa kuelewa nini kimetokea huku umiliki wa eneo hilo ukisoma kwa jina la kanisa la EAGT

Mchungaji Boaz Kazeba ndiye anadaiwa kubadilisha kanisa hilo la EAGT na kuwa AGGCI lililopo eneo la Bugarika mtaa wa Zahanati kata ya Pamba jijini Mwanza

"Sikutaka nifanye kitu chochote kile lakini umesikia wameniita mimi gaidi sijui muhuni, elishababu sijui nashangaa na huyo aliyesema mimi ni muumini wangu wa zamani anayosema ametoa kiwanja ana vielelezo? Hapa sisi tulimjengea mtu nyumba ya vyumba vitatu na maandishi ninayo siyo kama nazungumza kitu ambacho hakipo" ameeleza mchungaji Boaz

Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Zahanati Mashaka Nkonyoka amesema bado kanisa hilo lipo chini ya umiliki wa EAGT

"Lakini kimsingi kanisa hilo linaendeshwa na EAGT kama waanzilishi wa kanisa hilo siku zote ipo hivyo sasa imetokea kama wiki moja iliyopita mchungaji wa kanisa hilo Boazi Kazeba kubadilisha jina la kanisa hilo kutoka EAGT  na kuwa AGGCIA yani kanisa jipya"

Hadi EATV inatoka katika eneo hilo bado kanisa hilo lilikuwa limefungwa huku viongozi wa pande zote mbili wakipelekwa polisi kwa ajili ya mahojiano ili kutafuta suluhu ya mgogoro huo
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi