Jumatatu , 19th Dec , 2022

Watu watano wamefariki dunia na wengine kujeruhiwa baada ya kuangukiwa na jengo walilokuwa wakilijenga kwenye Kijiji Cha Sembeti  Marangu wilayani Moshi mkoani Kilimanjaro.

Wakati zoezi la uokoaji likiendelea  imebainika kuwa watu 30 walikuwa miongoni mwa watu  waliokuwa wakihusika na ujenzi wa jengo la ghorofa mbili lililoporomoka Jana jioni katika Kijiji cha Sembeti wilayani Moshi mkoani Kilimanjaro
Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Kilimanjaro Simoni maigwa amedhibitisha kutokea kwa tukio hilo.

Mkuu wa wilaya ya moshi abasi kayanda amezunguzia tukio hilo na kuwataka wananchi mkoani hapa kufuata sharia na kanuni wakati wa kufanya ujenzi ikiwa ni pamoja na upimwaji wa eneo husika kwani sio kila eneo linastahili kujengwa ghorofa