Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Watatu wakamatwa na Jeshi la Polisi

Jumatano , 14th Feb , 2018

Jeshi la Polisi mkoa wa Mbeya limewakamata vijana watatu maeneo ya Mwanjelwa, Kata ya Ruanda Tarafa ya Iyunga Jijini Mbeya wakiwa na nyara za serikali ambazo ni vipande vinne vya meno ya Tembo.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoani humo DCP Mohammed Mpinga amesema mnamo Februari 05, 2018 majira ya 1:45 usiku walifanikiwa kuwakamata vijana hao waliotambulika kwa majina ya Kenedy Lupembe Simsokwe (43) ambaye ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha SAUT tawi la Mbeya na mkazi wa Iyela, Mathew Elikana Mwanjala (42) mpiga picha pamoja na Shaban Mkwiche (24) mkazi wa Iyunga.

Aidha, Kamanda Mpinga amesema baada ya kukamatwa na kupekuliwa watuhumiwa hao walikutwa na nyara hizo ambavyo vina uzito wa kilogram 5 vyenye thamani ya Tshs Milioni 33.

Kwa upande mwingine, DCP Mpinga amesema taratibu za kisheria zinafanyika ili watuhumiwa wafikishwe mahakamani kwa hatua zaidi, huku akiwataka wananchi kuacha tabia ya kuwa na tamaa ya kujipatia utajiri wa haraka kwa kutumia njia za mkato zisizo halali, badala yake wafanye kazi halali ili kupata kipato halali. 

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa