Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Watoto kupata taarifa za matukio ya ukatili

Jumamosi , 28th Jan , 2023

Jeshi la Polisi mkoani Arusha limeungana na watoto wanaoishi katika kituo cha kulelea yatima kijulikanacho kwa jina la Maasai Girls Rescue Center kilichopo wilaya ya Karatu kwa lengo la kuwaleta karibu watoto na jeshi hilo ili kupata taarifa za matukio ya ukatili wa kijinsia.

Baadhi ya Askari wa Jeshi la Polisi Arusha wakiwa na watoto yatima

Tukio hilo limefanyika leo Januari 28, 2023, Mkuu wa polisi wilaya ya Karatu Mrakibu Mwandamizi wa Polisi SSP Radegunda Marandu, amesema jeshi hilo limetoa misaada mbalimbali kwa yatima hao ikiwa ni mkakati wa kuifanya jamii kuwa karibu nao.

SSP Marandu amebainisha kuwa pamoja na kuwa jeshi hilo linahusika na ulinzi wa raia na mali zao pia wanalo jukumu la kushirikiana na wananchi katika matukio  ya kijamii ikiwemo la kuonyesha upendo kwa yatima ambapo watakua huru kueleza changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwemo za ukatili.

Sambamba na hilo pia ametoa onyo kwa watu wachache ambao wana tabia ya kuwafanyia watoto vitendo vya ukatili kuacha mara moja kwani jeshi hilo lipo makini na litachukua hatua kali za kisheria dhidi yao.

Naye Bwana Elisante Loi, meneja wa kituo hicho amesema msadaa uliotolewa utawafanya watoto hao kujua kuwa polisi ni sehemu ya jamii hivyo watakua huru kueleza changamoto mbalimbali zinazowakabili kwa jeshi hilo bila kuogopa.
 

HABARI ZAIDI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa