Jumamosi , 17th Sep , 2022

Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia watoto na wanawake  UNICEF , limesema kwamba mafuriko makubwa nchini Pakistan yamesababisha takribani watoto milioni  3.4 kuhitaji msaada wa haraka wa kuokoa maisha yao .

 

 

Mafuriko hayo yaliyosababishwa na mvua kubwa yametajwa kama janga kubwa la kibinadamu  kuwahi kutokea nchini humo ndani ya miaka 10 iliyopita. Shirika la kuhudumia watoto UNICEF limesema takribani watoto 16 wameathiriwa na janga hilo.

Kitengo cha maafa nchini Pakistan kinakadiria kwamba katika kipindi cha kuanzia katikati ya mwezi Juni  vifo vitokanavyo na mafuriko hayo vimefikia    1,545 ambapo kati ya vifo hivyo 552 ni watoto.

Mamlaka zinasema kwamba huenda idadi ya vifo ikaongezeka kutokana na uwepo wa magonjwa ya homa kali homa ya dengue .