Jumatatu , 19th Sep , 2022

Jumla ya watu 6 wamepoteza maisha na wengine 20 kulazwa katika hospitali ya Wilaya ya Kiteto Mkoani Manyara, kufuatia ajali ya basi lililoanguka katika kijiji cha Chekanao, huku chanzo cha ajali hiyo kikitajwa kuwa mwendokasi wa dereva.

Basi lililopata ajali

Akithibitisha kutokea kwa ajali hyo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara (RPC) George Katabazi amesema ajali hiyo imetokea asubuhi ya leo Septemba 19.2022 ikihusisha basi lenye namba za usajili  T 266 APF aina ya mistubish minebas lililokuwa likitokea Matui Wilayani Kiteto kwenda Wilaya ya Kondoa Mkoani  Dodoma.

RPC Katabazi amefafanua kuwa kati ya majeruhi ishirini wa ajali hiyo, majeruhi watatu wamesafirishwa kwenda Dodoma kwa matibabu zaidi.