Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Watumishi serikalini wachota bilioni 1.34

Ijumaa , 15th Mar , 2019

Mkuu wa mkoa wa Rukwa, Mh. Joachim Wangabo ametoa siku saba kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa, kuhakikisha anaunda timu ya uchunguzi ili kuwabaini wadaiwa wa shilingi bilioni 1.34 za makusanyo ya mapato.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Mh. Joachim Wangabo

Amesema hayo baada ya kupitia taarifa za makusanyo na kubaini tatizo la kutowasilishwa kwa makusanyo ya mapato ya ndani kwa kutumia mfumo wa Local Governent Revenue Collection Information System (LGRCIS) na kueleza kuwa kumekuwa na watendaji ambao sio waaminifu wanaokabidhiwa makusanyo hayo  na kuyaingiza kwenye matumizi binafsi.

Amesema watumishi hao huzitumia pesa hizo katika biashara zao wakitegemea kurudisha na matokeo yake bili za wakusanyaji hazikubali kutoka kwenye mfumo hadi fedha zote alizokusanya zitimie.

Akitolea mfano Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi Mh. Wangabo amesema kuwa, “hadi kufikia mwezi Februari mwaka 2019, jumla ya Shilingi Milioni 98 zimetumika kama sehemu ya gharama za wakusanyaji baada ya kuzikata na kutumia. Matokeo yake fedha zinapelekwa halmashauri zikiwa pungufu na kuongeza kuwa jumla ya shilingi 241 za halmashauri hiyo zilitumika kabla ya kupelekwa benki jambo hilo ni kinyume na kifungu cha 32 cha Memoranda ya Fedha za Serikali za Mitaa”.

Alitoa agizo hilo wakati wa ufunguzi wa semina ya mafunzo elekezi kwa waheshimiwa madiwani kutoka katika halmashauri zote nne za Mkoa wa Rukwa iliyofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Sumbawanga ambapo Mh. Wangabo alikuwa mgeni rasmi wa semina hiyo.  

Akitoa neno la Shukurani kwa mgeni rasmi mstahiki Meya wa manispaa ya Sumbawanga alipongeza juhudi za mkuu wa mkoa wa Rukwa kuhakikisha anasimamia vyema maendeleo ya mkoa huo, na kumuhakikishia kuwa hawatamuangusha katika kuhakikisha ukusanyaji wa mapato unaongezeka.

Hadi kufikia tarehe 12 mwezi Machi mwaka 2019, Manispaa ya Sumbawanga ina wadaiwa wa makusanyo ya mapato ya ndani shilingi milioni 45.97, Sumbawanga Vijiji Shilingi Milioni 756.17, Wilaya ya Kalambo Shilingi Milioni 252.64 na Wilaya ya Nkasi Shilingi Milioni 290.95.

Bonyeza hapa chini kutazama zaidi.
 

HABARI ZAIDI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa