Jumanne , 8th Dec , 2020

Mbunge wa jimbo la Iringa Mjini, Jesca Msambatavangu amesema wameshakutana na wazee wa kimila katika jimbo hilo na kukubaliana kushirikiana kwa ajili ya kutokomeza mila potofu zinazochangia kwenye matukio ya ukatili wa kijinsia.

Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini, Jesca Msambatavangu

Akizungumza katika mahojiano, na Kipindi cha Supa Breakfast, Jesca amesema masuala ya matukio ya ukatili wa kijisia ni masuala mtambuka ambayo yanahusu jamii nzima kiujumla

"Yapo mambo ambayo yanasababisha huu ukatili unaendelea zipo mila potofu kama ukeketaji, mtoto wa kike hawezi kuamua anaamuliwa na wazazi wake, tumekutana na viongozi wa kimila na tumeongea nao na wao wamekubali kuanzia sasa wataanza kutoa elimu na kushirikiana na serikali kupambana na mila potofu" amesema Jesca

Aidha Jesca amesema ili kudhibiti suala hilo zipo sheria za ndoa ambazo inabidi zifanyiwe mabadiliko huku akielezea mikakati wanayoifanya katika jimbo lake kupambana na ukatili wa kijinsia.

"Kikubwa tunachokifanya jimbo la Iringa ni kuhakikisha wadau wote wanaohusika wamehamasishwa vya kutosha na wamepata elimu ya kutosha kujua majukumu yao" amesema Jesca