Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Waziri Kabudi apingwa hadharani, makundi yaungana

Jumanne , 5th Mar , 2019

Baada ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof Palamagamba Kabudi kuwataka Watanzania kuwa wazalendo na nchi yao na kutoisema vibaya au kuidhihaki, amekosolewa na makundi mbalimbali ya kijamii wakisema serikali itaendelea kusemwa vibaya na siyo nchi.

Waziri wa Mambo ya Nje, Prof. Kabudi

Baada ya kauli hiyo, mjadala mzito umezuka kwa viongozi na watu mbalimbali katika mtandao wa Twitter wakidai kwamba katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali haijatajwa kama ni nchi.

Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe amesema kwamba yeye ataendele kusema mabaya ya serikali ya nchi yake popote na wakati wowote.

"Ninaipenda sana nchi yangu Tanzania. Nimeitumikia kwa weledi kila nipatapo nafasi ya kufanya hivyo. Nimeilinda nchi yangu dhidi ya majaribu mbali mbali. Nitaisema vibaya Serikali ya Nchi yangu popote na wakati wowote inapofanya Mambo kinyume ya misingi ya katiba ya Tanzania," Zitto Kabwe.

Rapa wa muziki wa Bongo Fleva, Webiro Wasira "Wakazi' amesema kwamba Wanaoisema nchi siyo watanzania lakini kwa upande wake atazidi kuikosoa serikali pale inapoenda tofauti.

"Professor PK anafahamu hili, na inathibitishwa kwa matamshi yake na msisitizo wake. Anajaribu sana, maskini. Wanaoweza kuisema nchi yetu sio sisi, labda ungewa address kwa English. Ila mimi nitaendelea kuisema Serikali ikizingua kama kawaida," Wakazi.

Mwanasheria Jebra Kambole amesema kwamba,  "tofautisha nchi na serikali!! Nchi hatutaisema vibaya maana nchi ni wananchi, tutaitetea Daima!!! Lakini tutaisema na kuibagaza kadili Mungu atakavyotupa uhai!!!. Yani tutaibagaza serikali aseeeeeee!".

Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu amesema kwamba  Profesa Kabudi  ajulishwe kwamba hawatanyamazishwa na uovu wao, au vitisho vyao, au  ulaghai na propaganda zao, au na hongo na rushwa zao.

"Mwambieni Profesa Kabudi kwamba tutaendelea kuyasema hadharani, popote pale, ndani na nje ya Tanzania, maovu ya Serikali yetu, na ya vyombo vyake, na ya viongozi wake na ya watendaji wake", amesema Lissu.

HABARI ZAIDI

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ