Jumamosi , 2nd Oct , 2021

Aliyekuwa Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji, na Mbunge wa Ngorongoro William Tate Ole Nasha, leo Oktoba 2, 2021, amepumzishwa kwenye makazi yake ya milele kijijini kwake Osinoni wilayani Ngorongoro.

Waziri MKuu Kassim Majaliwa, akiweka mchanga kwenye kaburi la aliyekuwa Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji, na Mbunge wa Ngorongoro William Tate Ole Nasha

Mazishi hayo yamehudhuriwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Spika wa Bunge Job Ndugai, wananchi, ndugu jamaa na marafiki pamoja na viongozi wengine wa serikali

Ole Nasha alifariki dunia Septemba 27 mwaka huu jijini Dodoma, na taarifa zilieleza kwamba kifo chake kilisababishwa na shinikizo la damu,