Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Waziri mkuu ataja watakaohusika uchaguzi Mkuu 2020

Alhamisi , 18th Jul , 2019

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, amewataka vijana waliotimiza umri wa kupiga kura wajitokeze kwa wingi katika zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la mpiga kura.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa

Waziri Mkuu ameyabainisha hayo leo Julai 18, wakati wa uzinduzi wa daftari hilo Mkoani Kilimanjaro.

"Nitoe rai kwa vijana wote wa Kitanzania, waliotimiza umri wa miaka 18, au wale ambao watatimiza umri huo ifikapo Oktoba, 2020, wajitokeze kwa wingi na kujiandikisha, katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, hawa ndio walengwa wakuu kwa sababu wanaingia kwa mara ya kwanza katika uchaguzi." amesema Waziri Mkuu.

Ambapo amesema kwamba, bila kujiandikisha hawataweza kutumia haki yao ya msingi, ya kuchagua viongozi wanaowataka, hivyo kujiandikisha kwao kutawahakikishia ushiriki wao, katika uchaguzi wa viongozi.

Amesema zoezi hilo ambalo limeanza leo, linafanyika kwa mara ya kwanza tangu kumalizika, kwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2015. zoezi ambalo litafanyika nchi nzima, na linatarajiwa kukamilika Machi, 2020.

"Watakaohusika awamu hii ni wapigakura waliotimiza miaka 18 hivi karibuni, wale watakaotimiza miaka 18 wakati wa Uchaguzi Mkuu Oktoba 2020, waliohama kata au Jimbo na kuhamia maeneo mengine ya kiuchaguzi, waliopoteza kadi au kadi zao kuharibika, wanaohitaji kurekebisha taarifa zao, mfano majina ambayo hapo awali yalikuwa yamekosewa, sambamba na kuwaondoa wapiga kura waliopoteza sifa kama vile kufariki," amesema.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa