
Waziri George Simbachawene
Mhe. Simbachawene, ameitikia agizo hilo kwa kuwataka wakuu wa wilaya pamoja na halmashauri zote nchini kuangalia ufumbuzi na utaratibu mzuri wa kuwashirikisha wajasiriamali hao ili kupata ufumbuzi ulioshirikisha kuliko utaratibu wa sasa wakuwafukuza bila kusikiliza madai yao.
Mhe. Simbachawene amesema, Rais Magufuli anatambua mchango mkubwa na kazi nzuri inayofanywa na wakuu wa wilaya katika kuleta maendeleo hivyo kuweka maeneo sahihi kwaajili ya wafanyabiashara wadogo kutaleta maana kubwa ya uwajibikaji.
Hivi karibuni waziri huyu alitoa agizo kwa wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya nchi nzima kuhakikisha wanawaondoa wafanyabiashara hao katika maeneo yasiyo rasmi agizo ambalo lilianza kutekelezwa mara moja katika maeneo mbalimbali ikiwemo Mwanza na Dar es Salaam.