Ijumaa , 26th Aug , 2022

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki, amewahimiza wawekeza kutoka sekta binafsi nchini kuwekeza katika sekta ya mifugo kwa sababu kuna fursa kubwa ya kukuza mitaji yao na kupata faida.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki

Kauli hiyo ameitoa alipotembelea na kukagua maendeleo ya kiwanda cha kuchakata maziwa na chakula cha mifugo kilichopo wilayani Karagwe, mkoani Kagera na kuwahimiza wawekezaji wa sekta binafsi kuwekeza katika sekta ya mifugo nchini kwa sababu inawezekana.

"Niseme tu kwamba sisi Wizara ya Mifugo tuko tayari kumuunga mkono mwekezaji yeyote atakayeweza kufanya uwekezaji mahiri kama alivyofanya Kahama Fresh ili  shughuli ya ufugaji iwe ya  kibiashara zaidi na kuleta tija kwao binafsi na Taifa kwa ujumla," amesema Waziri Ndaki

Aidha Waziri Ndaki ameongeza kuwa wawekezaji binafsi wakiwekeza katika sekta ya mifugo na kufanya ufugaji wa kibiashara watasaidia kuongeza fursa za ajira kwa wananchi lakini pia watakuza pato la Taifa.