Jumatano , 27th Jan , 2016

Bunge la Kumi na Moja limewachagua wenyeviti wa tatu wa bunge ambao watasaidiana na spika wa bunge na naibu spika katika kuliongoza bunge la kumi na moja katika kipindi cha nusu ya uhai wake.

Waliochaguliwa ni mwenyekiti wa kamati ya sheria ndogo Andrew Chenge (MB), mwenyekiti wa kamati ya ardhi, maliasili na utalii Dr Mary Mwanjelwa (MB) na makamu mwenyekiti wa kamati ya sheria na Katiba Najma Giga (MB).

Aidha Spika wa bunge Job Ndugai amewaita wagombea wote watatu kujinadi mbele ya Bunge kabla ya kupigiwa kura ya pamoja ya Ndio au Hapana.

Ambapo wenyekiti wa kamati ya sheria ndogo Andrew Chenge (MB), mwenyekiti wa kamati ya ardhi, maliasili na utalii Dr Mary Mwanjelwa (MB) na makamu mwenyekiti wa kamati ya sheria na katiba Najma Giga (MB) wamechaguliwa kwa kura nyingi za ndio kuwa wenyeviti wa bunge.