Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wizara zote zatakiwa Dodoma kabla ya Feb. 28

Alhamisi , 19th Jan , 2017

Serikali imezipa msisitizo wizara mbalimbali kuhakikisha zinahamishia makazi yake Makao Makuu ya nchi mkoani Dodoma kabla ya Februari 28, mwaka huu, kama iliyotangazwa na Rais John Magufuli mwaka jana.

Waziri Jenista Mhagama wakati wa kufungua mkutano mkuu wa mwaka wa wanachama wote wa Saccos ya Makamu Savings and Credit iliyopo chini ya ofisi ya Wziri Mkuu, leo Mjini Dodoma

 

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Ulemavu, Jenista Mhagama, alisema agizo la serikali lazima liwe limetekelezwa ifikapo Februari 28, mwaka huu.

“Kama agizo lilivyotolewa na Rais Magufuli kuhusu wizara na watumishi wake kuhamia Makao Makuu Dodoma, ndivyo wanavyotakiwa manaibu makatibu wakuu, makatibu, manaibu mawaziri na mawaziri kutakiwa kuwapo Dodoma mwishoni mwa Februari,” alisema Mhagama.

Waziri Mhagama alisema ofisi yake imeweza kukagua miundombinu na ujenzi wa majengo mbalimbali ya serikali yanayoendelea kujengwa na mengine yakiwa yamekamilika kwa ajili ya matumizi ya wizara hizo.

“Hakuna tatizo la ofisi za watumishi wa wizara zote, kwani majengo yamekamilika na yapo katika hali nzuri tayari kwa ajili ya kuanza kutumiwa, hivyo wakuu husika wakiwamo mawaziri wahakikishe wanatakiwa kuhamia Dodoma,” alisema.

 

 

HABARI ZAIDI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa