Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ziwa Kisiba na uwepo wa nyoka mwenye vichwa viwili

Jumanne , 10th Sep , 2019

Ziwa masoko au Kisiba linapatikana Mkoani Mbeya katika Wilaya ya Rungwe umbali wa Kilomita 19 kufika eneo hilo ukitokea Tukuyu Mjini.

Ziwa masoko au Kisiba.

Kuna masimulizi mengi kuhusu Ziwa hilo mengi yakiwa ya Kitamaduni zaidi, na hii ndiyo huvutia watu wengi kwenda kutalii. Inaaminika wakati wa Vita ya Kwanza ya Dunia wakati Wajerumani wakiondoshwa walificha masanduku ya mali nyingi za thamani katika Ziwa hilo.

Mpaka sasa inaelezwa mali hizo zipo lakini hakuna ambaye ameweza kuzichukua kwa kile kinachodaiwa uwepo wa nguvu za ajabu pamoja na Nyoka mkubwa mwenye vichwa viwili ambae analinda mali hizo.

Akizungumza na EATV & EA Radio Digital, Mratibu Mkuu wa Everyday Mbeya, Taasisi inayohusika na kuwatembeza Watalii mbalimbali ndani ya Mkoa huo, Shah Mjanja anasema stori hizo ni masimulizi lakini hakuna uthibitisho wowote wa uwepo wa mali hizo.

"Nimewahi kufanya utafiti kidogo binafsi ni kweli kuna baadhi ya watu wanasema ukiogelea kwenda chini sababu Ziwa lina kina kifupi tu kama mita 70, unaweza kuona masanduku ya kale ambayo yanahusishwa na hiyo ishu ya Wajerumani," alisema.

Aidha simulizi nyingine inaelezea kuwa Ziwa hilo lilitokea ikiwa ni ufunuo aliopata mtu mmoja ambaye inasemekana alitokea Malawi.

Mtu huyo aliomba maji ya kunywa lakini wenyeji wa eneo hilo walimnyima lakini alitokea mtu mmoja ambaye alimpatia maji na ndipo akamwambia mtu aliyempatia maji kuwa aondoke eneo hilo sababu kesho yake eneo zima litatawaliwa na maji, ndiyo chanzo cha Ziwa hilo.

“Kuna Masimulizi mengi kwa mdomo, na kama unavyojua kwa waswahili linalozungumzwa sana huenda lipo lakini sisi hatupo sana huko kwa sababu yanavuruga utalii lakini masimulizi hayo yapo kweli,” aliongeza zaidi.
 

HABARI ZAIDI

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani