Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Nitafanya dhambi ya kuvunja nyumba" - Lukuvi

Jumatatu , 23rd Oct , 2017

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi, William Lukuvi ameweka wazi mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Magufuli kwamba yupo radhi kufanya dhambi ya kuvunja nyumba za watu waliovamia kwenye eneo la mtanzania mnyonge ili eneo lirudi kwa

muhusika halali.

Waziri Lukuvi amebainisha hayo leo Ikulu Jijini Dar es salaam, baada ya Rais Magufuli kumaliza kuwapatia vyeti wanakamati waliofanya mazungumzo na kampuni ya Barrick Gold na wale waliofanya uchuzi wa thamani katika makinikia.

Amesema kwamba serikali haitawafumbia macho wavamiaji ambao wanawaonea wamiliki halali wa ardhi kwakuwa wao hawana pesa za kupambana nao kwa sababu wakati anakabidhiwa nafasi ya kuongoza wizara hiyo Mh. Rais alimuambia aende akawasaidie wanyonge.

Nitafanya dhambi ya kuvunja nyumba ya yule aliyevamia eneo la mwingine ili haki kamili irudi kwa mmiliki halali. Nilipokuwa Sumbawanga juzi Mbunge aliniambia viongozi wote wa Mkoa wameshindwa. Watu wababe wanatokea na kujenga kwenye viwanja vya watu maskini wale walio na hati ya umiliki. Serikali haitawafumbia macho wavamiaji kuwaonea wenye umiliki.

"Uliniambia niende wizara ile nikaondoe uonevu, kuna ukiukwaji mkubwa wa sheria. Nipo kuhakikisha uonevu unakoma. Lazima nyumba zao tuziwekee alama ya X na tutazivunja. Lazima masikini wapatiwe haki zao. Japo najua changamoto ni nyingi na kwenye hii wizara kama unavyojua utajiri upo nje nje kwa sababu ya dhuluma niwaambie hatutawavumilia. Serkali tutasimama kuondoa ulaghai na wale wenye kujenga kwa kutumia mabavu tutawaondoa". Lukuvi

Ameongeza "Sitawafumbia macho watakaopora viwanja halali vya maskini kwa kuwa wao wanapesa, tutazivunja nyumba zao na miliki itarudishwa kwa mwenye nayo".
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi