
Pichani Ofisi ya Chadema
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwenye ukurasa wa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, (CHADEMA) watuhumiwa hao waliachiwa siku ya jana tarehe 23/11/2020 usiku huku wakitaja sababu yakuachiwa kuwa upande wa Jamhuri haupo tayari kuendelea na kesi hiyo.
Nusrat Hanje, Mwaipaya pamoja na wenzao sita walikuwa wanakabiliwa na tuhuma zakufanya mikusanyiko isiyo ya halali , kudharua wimbo na bendera ya taifa .
Aidha kwa mujibu wa taarifa ya CHADEMA wanasiasa hao wanaachiwa huru wakiwa wametimiza siku 133 Gerezani huku wakiachiwa huru kabla ya maamuzi ya rufaa yao ambayo ilitakiwa isikilizwe tarehe 25/11/2020.