Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Aliyemfungia Wema Sepetu atumbuliwa

Alhamisi , 25th Apr , 2019

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bi. Susan Mlawi ameagizwa ampangie kazi nyingine Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Filamu na Michezo ya Kuigiza, Bi. Joyce Fisoo na ateue mtu mwingine kushika nafasi hiyo. 

Kutoka kulia ni Joyce Fisoo akizungumza na Wema Sepetu ambaye alikuwa na Katibu wake Neema Ndepanya katikati

Agizo hilo lilitolewa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, wakati akihitimisha kikao chake na wasanii zaidi ya 100 kutoka Shirikisho la Filamu Tanzania kilichofanyika ukumbi wa Hazina, jijini Dodoma. 

Kikao hicho ambacho kilidumu kwa zaidi ya saa saba, kilihudhuriwa na viongozi waandamizi kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bodi ya Filamu Tanzania pamoja na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) wakiongozwa na Naibu Waziri wa Habari, Juliana Shonza.

 “Katibu Mkuu mtafutie eneo jingine la kufanya kazi. Hana tuhuma zaidi ya mahusiano mabaya na wadau wake, ana historia nzuri, lakini tatizo ni mahusiano. Mpeleke idara nyingine na hapa mlete mtu mwingine", ameagiza Waziri Mkuu.

Amesisitiza kuwa, "Mama Fisoo wewe uko 'clean', sina tatizo na utendaji wako lakini ukikaa hapa hutaweza kwenda mbele na wala hawa wote hawatakuja kufanya kazi na wewe. Tunataka hii tasnia iende mbele, tunataka maendeleo kwenye tasnia ya filamu".

Shirikisho la Filamu Tanzania linajumuisha vyama 11, ambapo 10 vimesajiliwa na kimoja hakijakamilisha usajili. Vyama hivyo ni vya waigizaji, waongozaji, watayarishaji, wahariri, wachekeshaji na wapigapicha. Wengine ni waandishi wa miswada (script writers), watafutaji mandhari, wasambazaji wa filamu, walimu na chama cha wanawake wa tasnia ya filamu ambacho bado kiko kwenye mchakato wa usajili.

Joyce Fisoo alimfungia Wema Sepetu kwa muda wa miezi kadhaa baada ya kuvuja kwa picha zake za faragha mtandaoni, kitendo kilichoonesha kutowafurahisha wasanii wa filamu ambao mwishoni mwa wiki iliyopita walikuwa na kikao cha dharura wakishinikiza aondolewe.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya